Namna gani tuna pashwa kusali

ENSEIGNANT : Paulin CHOKORO NDERHE

Passage biblique à lire : Matthieu 5 : 15

Thème : Namna gani tuna pashwa kusali

 

Version swahili

1.   UKUMBUSHO WA SOMO LA SIKU YA TATU (LILILO TOLEWA NA MWALIMU ZALUMIRE)

Je, ni wangapi leo huomba ili wapate vitu? Wengi wetu, kwa masikitiko, ndio hivyo.

Yesu alivunja aina mbili za sala zisizo za kweli:

·        Sala ya unafiki (kuomba ili kuonekana),

·        Sala ya kipagani (kuomba ili kupata vitu kwa kulazimisha).

Katika hotuba (Ce discours) hii, Yesu anaeleza sala ya kweli:

Ni kilio cha mtoto kwa Baba yake, (Un cri d’enfant au Père)

kinachomlenga Mungu, (Centré sur Dieu)

huru kutokana na ubinafsi, (Libéré de l’Ego)

chenye imani kwa msaada wa Mungu, (Confiant dans la providence divine)

siyo mazoezi ya kidini. (Pas un exercice religieux)

 

Kusifiwa, kuonyesha "ukaribu wao wa kiroho" (Impressioner les autres) ; maneno ya kifahari, sala ndefu katika mikutano, wakichanganya maneno ya ajabu na yasiyoeleweka, wakidai ni "kunena kwa lugha" :  Lakini Mungu anachukizwa na haya. Yeye hamsikilizi muigizaji, anamsikiliza mtoto wake.

 

 

2.   SOMO LA SIKU

Mfano Halisi wa Sala: Kumlenga Mungu, Siyo Mtu

Yesu anafundisha sala tofauti kabisa na zile za kisasa:

Basi tusome hapo : Matayo 6 :9-13.

1.   Baba yetu uliye mbinguni → Siyo Mungu wa mbali, ni Baba wetu, aliye juu ya yote.

Baba anakaa mbiguni, (Zaburi 103 :19)

Amakuwa Baba yetu, nasi ni wana wake.  ( Warumi 8 :15 Roho mtakatifu hushuudiwa moyoni mwetu ya kwamba Mungu ni Baba Yetu)

1 Yohana 3 :1 ;  Zaburi 103 :13 ;

BWana mwenyewe ushuhudia : 2 wakorintho 6 :18.

 

2.   Jina lako litukuzwe → Lengo la kwanza siyo mafanikio yetu, ni utukufu wa Mungu.

Kusoma zaidi : Isaya 43 :7. Tuliumbwa kwa utukufu wa Bwana.

 

3.   Ufalme wako uje → Lengo siyo ufalme wetu, ni ufalme wa Bwana.

 

4.   Mapenzi yako yatimizwe duniani kama mbinguni → Siyo matakwa (mapenzi) yangu, bali mapenzi ya Baba.

 

Kila kitu kinaanza na Mungu. Siyo mimi.

Na baadaye ndipo tunaomba:

5.   Utupe leo riziki yetu ya kila siku → Si utajiri, bali kinachotosha leo tu.

Matayo 6:31-33

Musiseme, tutakula nini? Au tutakynya nini?.. bali utafuteni kwanza ufalme wa Mungu, na haki yake. Na hayo yote muta zidishwa.

Zaburi 37 :25 « Sijawayi kuona mwenye haki ameachwa, wala watoto wake wakiomba jiani »

6.   Tusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea → Sala inadai unyenyekevu (l’humilité), toba (La repentance), na msamaha (le pardon).

Matayo 18 :21-22 « Yesu akamwabia, si kukuambia hata mara saba, bali hata mara sabini mara saba »

 

7.   Usitutie majaribuni, bali utuokoe na yule mwovu → Kilio cha kutegemea Mungu katika udhaifu wetu.

2 Petro 2:9 “Bwana anajua kuwaokoa wacha Mungu na majaribu”

Akuna kile ambacho kina tu fikiya Bwana asiya ruhusu (Yobu 1:12)

Bwana hatatujaribu kupitia imani yetu ( 1 wakorintho 10:13)

8.   Kwa kuwa Ufalme ni Wako, Na nguvu, na utukufu hata milele amen

Ina mahanisha nini hapo!

Ufalme : Ya kwamba yeye ndiye ana mamlaka duniani na mbiguni : Zaburi 103:19. (L’autorité compétente)

Nguvu: Yakwamba tuna amini ya kuwa Mungu ndiye ana nguvu. Akuna kinacho tendeka bila uwezo wake. (Mambo ya nyakati 29:11).

Utukufu : Ya kuwa anakuwa anatukuzwa, na pia ana itaji kusifiwa.

-      Sifa zote,

-      Heshima

-      Na ushindi ni kwake.

Hata milele: yani iyo siyo mambo ya Muda, Ufalme wake niwa milele (Danieli 7:14).

Sharti la Sala: Kusamehe kwa Moyo

"Kama hamtasamehe wanadamu, Baba yenu hatawasamehe ninyi pia makosa yenu." (Mathayo 6:15)

Yesu anavunja udanganyifu huo: hakuna ushirika wa kweli na Mungu kama tuna chuki na kinyongo mioyoni mwetu.

 

Conclusion

Mkristo wa kweli haombi ili kumtawala Mungu.

Anaomba kwa sababu Mungu ni Baba yake — kwa upendo, kwa imani, na kwa unyenyekevu.

Lakini leo, sala nyingi zimekuwa kama amri (commandes) kwa Mungu:

·        "Natangaza, naamuru, natabiri..."

Wazimu huu ni nini? Wazimu kamili! (c’est de la folie, c’est contradictoire avec les écritures).

Je, sisi ni nani wa kumwamuru Muumba wa ulimwengu?

"Mapenzi yako yatimizwe."

Sala ya kweli ni kujisalimisha, siyo kudai.

 

SWALI KWA MUKUTANO

Utupe leo riziki zetu, je ni riziki za kiroho ama za kimwili ? ama ni zote mbili ??

Utusamehe makosa yetu, je ombi hili linakuwa tena (une déclaration de foi ??)

Katika mukutano ya wayahudi (katika utamaduni, dans la culture), kumuita Mungu Baba ilikuwa jambo la atuwa kubwa (un acte révolutionnaire), Je, ilikuwa tendo la imani ama la hatari ? na leo yii lina tu fundisha nini ?

Je tunawezaje ku iishi mufano huu bila ku vunja mantiki ya dunia ? (sans briser la logique du monde dominé par les injustices, la vengeance, ??)

 

Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

LEÇON : LE DERNIER ADAM, QUI EST-IL ?

POURQUOI ET COMMENT JESUS CHRIST PEUT ETRE 100% HOMME ET DIEU ?

Le Discours des Malheurs sur les Pharisiens (Matthieu 23) : Quand Jésus Détruit la Religion